Isaiah 7:1-9

Ishara Ya Imanueli

1 aWakati Ahazi mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, alipokuwa mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Aramu,
Yaani Shamu.
na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipanda kupigana dhidi ya Yerusalemu, lakini hawakuweza kuushinda.

2 cWakati huu nyumba ya Daudi iliambiwa, “Aramu wameungana na Efraimu.” Kwa hiyo mioyo ya Ahazi na watu wake ilitikiswa, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.

3 dNdipo Bwana akamwambia Isaya, “Toka uende, wewe na mwanao Shear-Yashubu,
Shear-Yashubu maana yake Mabaki Watarudi.
mkutane na Ahazi huko mwisho wa mfereji wa Bwawa la Juu, kwenye barabara iendayo Shamba la Dobi.
4 fMwambie, ‘Uwe mwangalifu, utulie na usiogope. Usife moyo kwa ajili ya watu hawa wawili walio kama visiki vya kuni vifukavyo moshi, kwa ajili ya hasira kali ya Resini na Aramu na ya mwana wa Remalia. 5 gAramu, Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga shauri baya ili wakuangamize, wakisema, 6 h“Tuishambulie Yuda, naam, tuirarue vipande vipande na kuigawa miongoni mwetu, na kumtawaza mwana wa Tabeeli awe mfalme juu yake.” 7 iLakini Bwana Mwenyezi asema hivi:

“ ‘Jambo hili halitatendeka,
halitatokea,
8 jkwa kuwa kichwa cha Aramu ni Dameski,
na kichwa cha Dameski ni Resini peke yake.
Katika muda wa miaka sitini na mitano,
Efraimu atakuwa ameharibiwa
kiasi kwamba hataweza tena kuwa taifa.
9 kKichwa cha Efraimu ni Samaria,
na kichwa cha Samaria
ni mwana wa Remalia peke yake.
Kama hamtasimama thabiti katika imani yenu,
hamtaimarika kamwe.’ ”
Copyright information for SwhNEN